Katibu Muhtasi (Personal Secretary II ) – Dar es salaam – Halmashauri Ya Wilaya Ya Misungwi

Kuajiriwa kwa waliohitumu kidato cha IV, waliohudhuria mafunzo ya Uhazili kutoka katika chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) au vyuo vinavyotambuliwa na serikali na kufaulu mitihani ya hatua ya tatu somo la Hati mkato ya Kiswahili na Hati makato ya Kiingereza maneno 80 kwa dakika na mafunzo ya kompyuta na kupata cheti katika program za WINDOWS, MICROSOFT OFFICE, INTERNET, E-MAIL NA PUBLISHER

JINSI YA KUTUMA MAOMBI
Maombi yote yatumwe kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa anuani ifuatayo

MKURUGENZI MTENDAJI (W)
S.L.P 20
MISUNGWI

MASHARTI YA JUMLA
(E) Awe raia wa Tanzania
(F) Awe mwenye maadili mazuri
• Hajafukuzwa kazi
• Hajapunguzwa kazi
• Hajafungwa na kupatikana na kosa la jinai
• Awe tayari kufanya kazi eneo lolote Misungwi bila kuhama kwa kipindi cha miaka 5
• Barua ya maombi iambatanishwe na picha (2) za sasa passport size na vivuli (photocopy) vya vyeti vya elimu na Taaluma
• Andika namba ya simu ya mkononi katika barua ya maombi ili kurahisisha mawasiliano

Mwisho wa kupokea maombi ni 30/05/2015 saa 9:00 alasiri

[yuzo_related]